Loading surah...
Back to Swahili Quran
49 Ayahs • Meccan
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَٱلطُّورِ
Naapa kwa mlima wa T'ur,
وَكِتَٰبٍۢ مَّسْطُورٍۢ
Na Kitabu kilicho andikwa
فِى رَقٍّۢ مَّنشُورٍۢ
Katika ngozi iliyo kunjuliwa,
وَٱلْبَيْتِ ٱلْمَعْمُورِ
Na kwa Nyumba iliyo jengwa,
وَٱلسَّقْفِ ٱلْمَرْفُوعِ
Na kwa dari iliyo nyanyuliwa,
وَٱلْبَحْرِ ٱلْمَسْجُورِ
Na kwa bahari iliyo jazwa,
إِنَّ عَذَابَ رَبِّكَ لَوَٰقِعٌۭ
Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.
مَّا لَهُۥ مِن دَافِعٍۢ
Hapana wa kuizuia.
يَوْمَ تَمُورُ ٱلسَّمَآءُ مَوْرًۭا
Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso,
وَتَسِيرُ ٱلْجِبَالُ سَيْرًۭا
Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.
فَوَيْلٌۭ يَوْمَئِذٍۢ لِّلْمُكَذِّبِينَ
Basi ole wao siku hiyo hao wanao kadhibisha,
ٱلَّذِينَ هُمْ فِى خَوْضٍۢ يَلْعَبُونَ
Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi.
يَوْمَ يُدَعُّونَ إِلَىٰ نَارِ جَهَنَّمَ دَعًّا
Siku watapo sukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu,
هَٰذِهِ ٱلنَّارُ ٱلَّتِى كُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ
(Waambiwe): Huu ndio ule Moto mlio kuwa mkiukanusha!
أَفَسِحْرٌ هَٰذَآ أَمْ أَنتُمْ لَا تُبْصِرُونَ
Je! Huu ni uchawi, au hamwoni tu?
ٱصْلَوْهَا فَٱصْبِرُوٓا۟ أَوْ لَا تَصْبِرُوا۟ سَوَآءٌ عَلَيْكُمْ ۖ إِنَّمَا تُجْزَوْنَ مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
Uingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyo kuwa mkiyatenda.
إِنَّ ٱلْمُتَّقِينَ فِى جَنَّٰتٍۢ وَنَعِيمٍۢ
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na neema,
فَٰكِهِينَ بِمَآ ءَاتَىٰهُمْ رَبُّهُمْ وَوَقَىٰهُمْ رَبُّهُمْ عَذَابَ ٱلْجَحِيمِ
Wakifurahi kwa yale aliyo wapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda na adhabu ya Motoni.
كُلُوا۟ وَٱشْرَبُوا۟ هَنِيٓـًٔۢا بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyo kuwa mkiyatenda.
مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ سُرُرٍۢ مَّصْفُوفَةٍۢ ۖ وَزَوَّجْنَٰهُم بِحُورٍ عِينٍۢ
Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyo pangwa kwa safu. Na tutawaoza mahuru-l-aini.
Page 1 of 3 (49 ayahs)