Loading surah...
Back to Swahili Quran
78 Ayahs • Meccan
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ ٱلرَّحْمَٰنُ
Arrah'man, Mwingi wa Rehema
عَلَّمَ ٱلْقُرْءَانَ
Amefundisha Qur'ani.
خَلَقَ ٱلْإِنسَٰنَ
Amemuumba mwanaadamu,
عَلَّمَهُ ٱلْبَيَانَ
Akamfundisha kubaini.
ٱلشَّمْسُ وَٱلْقَمَرُ بِحُسْبَانٍۢ
Jua na mwezi huenda kwa hisabu.
وَٱلنَّجْمُ وَٱلشَّجَرُ يَسْجُدَانِ
Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.
وَٱلسَّمَآءَ رَفَعَهَا وَوَضَعَ ٱلْمِيزَانَ
Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,
أَلَّا تَطْغَوْا۟ فِى ٱلْمِيزَانِ
Ili msidhulumu katika mizani.
وَأَقِيمُوا۟ ٱلْوَزْنَ بِٱلْقِسْطِ وَلَا تُخْسِرُوا۟ ٱلْمِيزَانَ
Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.
وَٱلْأَرْضَ وَضَعَهَا لِلْأَنَامِ
Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.
فِيهَا فَٰكِهَةٌۭ وَٱلنَّخْلُ ذَاتُ ٱلْأَكْمَامِ
Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.
وَٱلْحَبُّ ذُو ٱلْعَصْفِ وَٱلرَّيْحَانُ
Na nafaka zenye makapi, na rehani.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
خَلَقَ ٱلْإِنسَٰنَ مِن صَلْصَٰلٍۢ كَٱلْفَخَّارِ
Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo..
وَخَلَقَ ٱلْجَآنَّ مِن مَّارِجٍۢ مِّن نَّارٍۢ
Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
رَبُّ ٱلْمَشْرِقَيْنِ وَرَبُّ ٱلْمَغْرِبَيْنِ
Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
مَرَجَ ٱلْبَحْرَيْنِ يَلْتَقِيَانِ
Anaziendesha bahari mbili zikutane;
بَيْنَهُمَا بَرْزَخٌۭ لَّا يَبْغِيَانِ
Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane.
Page 1 of 4 (78 ayahs)