Loading surah...
Back to Swahili Quran
96 Ayahs • Meccan
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ إِذَا وَقَعَتِ ٱلْوَاقِعَةُ
Litakapo tukia hilo Tukio
لَيْسَ لِوَقْعَتِهَا كَاذِبَةٌ
Hapana cha kukanusha kutukia kwake.
خَافِضَةٌۭ رَّافِعَةٌ
Literemshalo linyanyualo,
إِذَا رُجَّتِ ٱلْأَرْضُ رَجًّۭا
Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,
وَبُسَّتِ ٱلْجِبَالُ بَسًّۭا
Na milima itapo sagwasagwa,
فَكَانَتْ هَبَآءًۭ مُّنۢبَثًّۭا
Iwe mavumbi yanayo peperushwa,
وَكُنتُمْ أَزْوَٰجًۭا ثَلَٰثَةًۭ
Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-
فَأَصْحَٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ مَآ أَصْحَٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ
Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?
وَأَصْحَٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ مَآ أَصْحَٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ
Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?
وَٱلسَّٰبِقُونَ ٱلسَّٰبِقُونَ
Na wa mbele watakuwa mbele.
أُو۟لَٰٓئِكَ ٱلْمُقَرَّبُونَ
Hao ndio watakao karibishwa
فِى جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Katika Bustani zenye neema.
ثُلَّةٌۭ مِّنَ ٱلْأَوَّلِينَ
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
وَقَلِيلٌۭ مِّنَ ٱلْءَاخِرِينَ
Na wachache katika wa mwisho.
عَلَىٰ سُرُرٍۢ مَّوْضُونَةٍۢ
Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.
مُّتَّكِـِٔينَ عَلَيْهَا مُتَقَٰبِلِينَ
Wakiviegemea wakielekeana.
يَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَٰنٌۭ مُّخَلَّدُونَ
Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,
بِأَكْوَابٍۢ وَأَبَارِيقَ وَكَأْسٍۢ مِّن مَّعِينٍۢ
Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.
لَّا يُصَدَّعُونَ عَنْهَا وَلَا يُنزِفُونَ
Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.
وَفَٰكِهَةٍۢ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ
Na matunda wayapendayo,
Page 1 of 5 (96 ayahs)