Loading surah...
Back to Swahili Quran
50 Ayahs • Meccan
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَٱلْمُرْسَلَٰتِ عُرْفًۭا
Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole!
فَٱلْعَٰصِفَٰتِ عَصْفًۭا
Na zinazo vuma kwa kasi!
وَٱلنَّٰشِرَٰتِ نَشْرًۭا
Na zikaeneza maeneo yote!
فَٱلْفَٰرِقَٰتِ فَرْقًۭا
Na zinazo farikisha zikatawanya!
فَٱلْمُلْقِيَٰتِ ذِكْرًا
Na zinazo peleka mawaidha!
عُذْرًا أَوْ نُذْرًا
Kwa kuudhuru au kuonya,
إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَوَٰقِعٌۭ
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa!
فَإِذَا ٱلنُّجُومُ طُمِسَتْ
Wakati nyota zitakapo futwa,
وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ فُرِجَتْ
Na mbingu zitakapo pasuliwa,
وَإِذَا ٱلْجِبَالُ نُسِفَتْ
Na milima itakapo peperushwa,
وَإِذَا ٱلرُّسُلُ أُقِّتَتْ
Na Mitume watakapo wekewa wakati wao,
لِأَىِّ يَوْمٍ أُجِّلَتْ
Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?
لِيَوْمِ ٱلْفَصْلِ
Kwa siku ya kupambanua!
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا يَوْمُ ٱلْفَصْلِ
Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini?
وَيْلٌۭ يَوْمَئِذٍۢ لِّلْمُكَذِّبِينَ
Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha!
أَلَمْ نُهْلِكِ ٱلْأَوَّلِينَ
Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia?
ثُمَّ نُتْبِعُهُمُ ٱلْءَاخِرِينَ
Kisha tukawafuatilizia walio fuatia?
كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِٱلْمُجْرِمِينَ
Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu!
وَيْلٌۭ يَوْمَئِذٍۢ لِّلْمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
أَلَمْ نَخْلُقكُّم مِّن مَّآءٍۢ مَّهِينٍۢ
Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa?
Page 1 of 3 (50 ayahs)