Loading surah...
Back to Swahili Quran
40 Ayahs • Meccan
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ عَمَّ يَتَسَآءَلُونَ
WANAULIZANA nini?
عَنِ ٱلنَّبَإِ ٱلْعَظِيمِ
Ile khabari kuu,
ٱلَّذِى هُمْ فِيهِ مُخْتَلِفُونَ
Ambayo kwayo wanakhitalifiana.
كَلَّا سَيَعْلَمُونَ
La! Karibu watakuja jua.
ثُمَّ كَلَّا سَيَعْلَمُونَ
Tena la! Karibu watakuja jua.
أَلَمْ نَجْعَلِ ٱلْأَرْضَ مِهَٰدًۭا
Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?
وَٱلْجِبَالَ أَوْتَادًۭا
Na milima kama vigingi?
وَخَلَقْنَٰكُمْ أَزْوَٰجًۭا
Na tukakuumbeni kwa jozi?
وَجَعَلْنَا نَوْمَكُمْ سُبَاتًۭا
Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?
وَجَعَلْنَا ٱلَّيْلَ لِبَاسًۭا
Na tukaufanya usiku ni nguo?
وَجَعَلْنَا ٱلنَّهَارَ مَعَاشًۭا
Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?
وَبَنَيْنَا فَوْقَكُمْ سَبْعًۭا شِدَادًۭا
Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?
وَجَعَلْنَا سِرَاجًۭا وَهَّاجًۭا
Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto;
وَأَنزَلْنَا مِنَ ٱلْمُعْصِرَٰتِ مَآءًۭ ثَجَّاجًۭا
Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni,
لِّنُخْرِجَ بِهِۦ حَبًّۭا وَنَبَاتًۭا
Ili tutoe kwayo nafaka na mimea,
وَجَنَّٰتٍ أَلْفَافًا
Na mabustani yenye miti iliyo kamatana.
إِنَّ يَوْمَ ٱلْفَصْلِ كَانَ مِيقَٰتًۭا
Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake,
يَوْمَ يُنفَخُ فِى ٱلصُّورِ فَتَأْتُونَ أَفْوَاجًۭا
Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi,
وَفُتِحَتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتْ أَبْوَٰبًۭا
Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango,
وَسُيِّرَتِ ٱلْجِبَالُ فَكَانَتْ سَرَابًا
Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.
Page 1 of 2 (40 ayahs)