Loading surah...
Back to Swahili Quran
46 Ayahs • Meccan
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَٱلنَّٰزِعَٰتِ غَرْقًۭا
Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,
وَٱلنَّٰشِطَٰتِ نَشْطًۭا
Na kwa wanao toa kwa upole,
وَٱلسَّٰبِحَٰتِ سَبْحًۭا
Na wanao ogelea,
فَٱلسَّٰبِقَٰتِ سَبْقًۭا
Wakishindana mbio,
فَٱلْمُدَبِّرَٰتِ أَمْرًۭا
Wakidabiri mambo.
يَوْمَ تَرْجُفُ ٱلرَّاجِفَةُ
Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,
تَتْبَعُهَا ٱلرَّادِفَةُ
Kifuate cha kufuatia.
قُلُوبٌۭ يَوْمَئِذٍۢ وَاجِفَةٌ
Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,
أَبْصَٰرُهَا خَٰشِعَةٌۭ
Macho yatainama chini.
يَقُولُونَ أَءِنَّا لَمَرْدُودُونَ فِى ٱلْحَافِرَةِ
Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?
أَءِذَا كُنَّا عِظَٰمًۭا نَّخِرَةًۭ
Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?
قَالُوا۟ تِلْكَ إِذًۭا كَرَّةٌ خَاسِرَةٌۭ
Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!
فَإِنَّمَا هِىَ زَجْرَةٌۭ وَٰحِدَةٌۭ
Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,
فَإِذَا هُم بِٱلسَّاهِرَةِ
Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!
هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ
Je! Imekufikia hadithi ya Musa?
إِذْ نَادَىٰهُ رَبُّهُۥ بِٱلْوَادِ ٱلْمُقَدَّسِ طُوًى
Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:
ٱذْهَبْ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ
Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.
فَقُلْ هَل لَّكَ إِلَىٰٓ أَن تَزَكَّىٰ
Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?
وَأَهْدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخْشَىٰ
Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.
فَأَرَىٰهُ ٱلْءَايَةَ ٱلْكُبْرَىٰ
Basi alimwonyesha Ishara kubwa.
Page 1 of 3 (46 ayahs)